Mfalme Lia
(Imetafsiriwa kutoka kwenye kitabu cha Tales From Shakespeare cha Charles na Mary Lamb, , cha 1805 )
LIA, mfalme wa Uingereza, alikuwa na binti watatu; Gonerili, mke wa Chifu wa Albani; Regani, mkewe Chifu wa Konwoli; na Kordelia, mwanamwali, ambaye Mfalme wa Ufaransa na Chifu wa Burgundi walikuwa wanataka kumchumbia, na walikuwa kwa wakati huu wako kwenye Jumba la Mfalme Lia kwa makusudi hayo.


